KWA NINI BIASHARA YAKO HAIFANIKIWI 1) Ni mwepesi wa kukata tamaa , unahisi biashara ndio imeshakufa na huna haja ya kujipanga tena kuiimarisha. Changamoto ndogo unashindwa kukabiliana nazo unakuwa mwepesi wa kuacha changamoto zikutawale badala ya kupambana nazo uzishinde. 2) Sio Mbunifu, Unashindwa kuwa mbunifu katika biashara unayoifanya na kufanya wateja wako waone hauna jipya. Tangu umefungua biashara yako hujawahi kufanya jambo lolote la utofauti ili kuongeza thamani na kuwavutia wateja. Wateja wameshachoka kuona kitu unachokiuza kila siku unatakiwa kuweka ubunifu ili kuongeza thamani na kufanya biashara yako kuwa mpya machoni kwa watu. 3) Hujaelewa wateja wako wanataka nini zaidi, unatumia nguvu nyingi, pesa na muda kufanya kile ambacho kinakupendeza wewe machoni na sio kinachowapendeza wateja. Kama bado hujalingundua hilo rudi sokoni chunguza wateja wanataka nini sio wewe unapenda nini. Cheza na soko linataka nini kwa wakati gani. 4) Huwajali wafanyakazi wako, ...
Posts
Showing posts from September 28, 2017
- Get link
- X
- Other Apps
NJIA RAHISI YA KUTANGAZA BIASHARA YAKO: Katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia matangazo (marketing) inabeba nafasi kubwa sana katika kufanya biashara imfikie mlaji kiurahisi na hivyo kuleta maendeleo katika biashara. Biashara za kukaa na kusubiri wateja waje zimepitwa na wakati, inatakiwa ubuni mbinu za kuwafuata wateja walipo. Nimeandika baadhi ya njia za kutangaza biashara, jaribu kuzifuata utaona matokeo. 1) Tengeneza vipeperushi na business cards, zisambaze kwa kila mtu unayeona anafaa kuwa mteja wako. 2)Tumia mitandao ya kijamii kujitangaza kama Facebook, Instagram 3)Tumia vyombo vya habari kama radio, televisheni na magazeti 4)Andaa matamasha utakayotumia kujitangaza 5)Hudhuria matamasha mbalimbali yaliyoandaliwa na utumie kujitangaza. 5)Tumia magari ya matangazo kutangaza huduma au bidhaa zako 6)Kuwa na utaratibu wa kuwa na siku ya punguzo la bei (promotion day) 7)Toa huduma iliyobora wateja wataletana wenyewe. (Good customer care) 8)Ajiri watu kwa ajili ya k...